Ndege ndogo ya abiria ambayo bado haijajulikana ni kampuni gani inadaiwa kuanguka katika Ziwa Victoria leo Alhamisi, Februari 23, 2023 na kuzua taharuki huku chanzo cha ajali hiyo kikiwa hakijajulikana bado.
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji tayari wamefika eneo la tukio na kuanza kutoa msaada ikiwa ni kuokoa abiria walikuwamo kwenye ndege hiyo kwa kushirikiana na wananchi wa eneo la karibu.
Kipande cha video ya tukio hilo kinaonyesha watu wakiokolewa majini huku ndege ikiwa imezama majini. Tayari magari ya kubeba wagonjwa yakipiga ving'ora yamefika eneo hilo na kubeba watu hao na kuwapeleka Hospitali.
Lakini inadaiwa kuwa huenda ni mazoezi ya uokoaji yanafanyika na Kikosi cha Uokoaji ili kujiweka tayari na matukio kama hayo endapo yakitokea.
Taharuki hiyo imetokea ikiwa ni miezi kadhaa tangu ajali ya ndege ya Shirika la Precision Air ilipoanguka katika Ziwa Victoria, Bukoba mkoani Kagera Novemba 6, 2022 na kuua watu 19, na kujeruhi 26 baada ya kushindwa kutua kutokana na hali mbaya ya hewa.
Tumefanya jitihada za kumtafuta Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza ili azungumzie tukio hilo lakini simu yake ya mkononi haipokelewi.
Aidha, taarifa ya mamlaka husika kuhusu tukio hilo bado haijatolewa. Endelea kufuatilia taarifa zetu kwa updates zaidi.
TAZAMA TUKIO HILO KWA KUBOFYA
Ndege ndogo ambayo bado haijajulikana ni kampuni gani inadaiwa kuanguka katika Ziwa Victoria leo na zoezi na uokoaji linaendelea kufanywa na vyombo vya uokoaji kwa ushirikiano na wananchi. MWANAHALISI online inaendelwa kufuatilia kwa taarifa zaidi pic.twitter.com/7Xh0jxZnoj
— MwanaHALISI Digital (@Mwanahalisitz) February 23, 2023
VIDEO:Taarifa iliyotufikia hapa MWANAHABARI DIGITAL Inasemekana kuna ndege nyingine imeanguka Muda huu ziwa Victoria Mwanza pic.twitter.com/7DZjXNJfq5
— MwanaHabari (@MwanaHabariNews) February 23, 2023
TAA YAKANUSHA: HAKUNA AJALI YA NDEGE MWANZA