Mon, 1 May 2023
Chanzo: Bbc
Video imeonekana ikionyesha tawi la Benki kuu ya Sudan likiungua moto huku mapigano yakiendelea kote mjini Khartoum.
BBC haijaweza kuthibitisha tarehe ambayo picha hii ya video ilichukuliwa.
Jumapili, mashambulio ya anga yaliongezeka katika mji huo licha ya kufikiwa kwa makubaliano yaliyolenga kuwaruhusu raia kukimbia.
Jeshi lilisema kuwa linaushambulia mji ili kuwatimua mahasimu wao wa jeshi la dharura - Rapid Support Forces (RSF).
Chanzo: Bbc
Related Articles: