Mapigano kati ya jeshi la Sudan na Wanajeshi wa kikosi cha RSF yaliongezeka siku ya Jumapili, wakati vita katika mji mkuu wa nchi hiyo na maeneo ya magharibi vikiingia wiki ya 12, bila dalili zozote za kumalizika kwa mzozo huo kwa amani.
Mashambulio ya anga na mizinga yalishuhudiwa, na milio ya silaha ndogo ndogo kusiskika, hasa katika mji wa Omdurman, na pia katika mji mkuu Khartoum, huku mzozo huo ukizidisha mzozo wa kibinadamu, na kutishia kuenea kuathiri maslahi mengine ya kieneo.
RSF ilisema iliangusha ndege ya kivita ya jeshi, na ndege isiyo na rubani huko Bahri, katika taarifa ambazo jeshi halikudhibitisha mara moja.
"Tunaogopa, kila siku mashambulisi yanazidi kuwa mabaya," Nahid Salah mwenye umri wa miaka 25, anayeishi kaskazini mwa Omdurman, alisema katika mahojiano ya simu na shirika la habari la Reuters.
RSF imedhibiti, kwa kiasi kikubwa, ardhi ya mji mkuu, na imeshutumiwa kwa uporaji na kuchukua nyumba kwa lazima, wakati jeshi likilenga zaidi, kufanya mashambulio ya anga na kutumia mizinga.
- Waziri Mhagama akabidhiwa sehemu ya uwanja wa Mashujaa
- Wafungwa 100 wa vita kuachiliwa katika siku ya Eid al-Adha
- Shambulizi la anga lasababisha vifo ikiwemo watoto Sudan
- Gavana wa jimbo la Darfur auwawa baada ya kuishutumu RSF
- Wakazi wa Khartoum wapaza sauti juu upungufu wa bidhaa muhimu
- Read all related articles