Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Gavana wa jimbo la Darfur auwawa baada ya kuishutumu RSF

Gavana Wa Jimbo La Darfur Auwawa Baada Ya Kuishutumu RSF Gavana wa jimbo la Darfur auwawa baada ya kuishutumu RSF

Fri, 16 Jun 2023 Chanzo: Voa

Mapigano yameendelea katika miji mbalimbali nchini Sudan Jumatano wakati vita vikiingia mwezi wa pili tangu kuanza.

Wakati huo huo vyanzo vya habari vinaeleza kuwa Gavana wa jimbo la Darfur ameuwawa baada ya kushutumu kupitia chombo cha habari kwamba vifo vya raia vimetekelezwa na kundi la wanamgambo.

Mzozo baina ya jeshi na kundi la wanamgambo la RSF limeshutumu mzozo wa kibinadamu huko Khartoum pamoja na miji mingine mikubwa katika majimbo ya Kordofan na Darfur.

Kuongezeka kwa wimbi la mapigano kunatishia kurefusha muda wa ghasia na kuteka makundi yenye silaha hasa yale yenye kufungamana na makabila pamoja na wahusika wa nje.

Gavana wa Darfur Magharibi Khamis Abubakar aliuwawa Jumatano na kundi lenye silaha aliloliongoza alisema saa chache baada ya kuishutumu RSF na wanamgambo washirika kwa mauaji ya kimbari.

Hakuna maelezo juu ya kifo chake yaliyotolewa, lakini vyanzo viwili vya serikali vilisema RSF inahusika .

Chanzo: Voa
Related Articles: