Mashambulizi zaidi ya makombora yameripotiwa katika mji mkuu wa Sudan Khartoum, huku mapigano kati ya majenerali wanaopigana nchini humo yakizidi.
Mshuhuda waliripoti moashambulio ya mizinga kuzunguka jengo la televisheni ya serikali katika mji unaopakana wa Omdurman.
Jeshi lilitangaza kuleta nguvu katika mji mkuu kutoka maeneo mengine ya Sudan.
Mapigano yameendelea kwa karibu wiki saba, kati ya jeshi la taifa na wapinzani wao wa kijeshi, huko Khartoum na eneo la magharibi la Darfur, licha ya juhudi za kusuluhisha mzozo huo.
Siku ya Alhamisi Marekani ilitoa vikwazo dhidi ya makampuni manne ya Sudan na watu kadhaa, baada ya kusambaratika kwa mazungumzo ya amani yaliyokuwa yakiongozwa na Marekani na Saudi Arabia.