Mwili wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa unatarajiwa kuzikwa Februari 17, mwaka huu kijijini kwao Ngarash wilayani Monduli Mkoa wa Arusha.
Lowassa amefariki dunia Februari 10, 2024 saa 8 mchana katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Makamu wa Rais, Dk Philip Mpango jana, Lowassa alifikishwa katika taasisi hiyo baada ya kuugua shinikizo la damu, matatizo ya mapafu na kujikunja kwa utumbo.
Taarifa kuhusu maziko yake, imetolewa leo Februari 11, 2024 na msemaji binafsi wa Lowassa, Aboubakar Liongo nyumbani kwa mwanasiasa huyo, Masaki jijini Dar es Salaam.
Amesema ratiba rasmi ya mazishi itaanza Februari 13, 2024 itakayohusisha taratibu zote za kiserikali.
"Taarifa zaidi kuhusu mazishi itatolewa baadaye, lakini kwa sasa maziko yatafanyika Ngarash Monduli mkoani Arusha siku ya Jumamosi, Februari 17, 2024 saa 8 mchana," amesema Liongo.
- Kisa cha Diana Chilolo kufuta namba ya Lowassa
- Tazama hapa msafara wa mwili wa Lowassa ukipelekwa Karimjee
- Shein, Sumaye waeleza uchapakazi wa Lowassa
- Picha: Matukio mbalimbali katika zoezi la kuaga mwili wa Lowassa
- Fredy Lowassa: Asingekuwa Rais Samia, baba asingefika juzi
- Read all related articles