Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema baada ya kuwasili msibani nyumbani kwa Marehemu Edward Lowassa na kusaini kitabu cha Maombolezo ametoa ratiba ya mazishi ambapo amesema katika Siku Tano za maombolezo Taifa litaendelea na shughuli za mazishi ya mpendwa wao na mazishi haya ni mazishi ya kitaifaa.
Amesema siku Jumanne, Februari 13, 2024 mwili utatolewa Lugalo kwenda ukumbi wa karimjee ambapo kutokuwepo na Ibada fupi baada ya hapo wananchi wataweza kupata nafasi ya kuaga mwili ambapo zoezi hilo litaenda mpaka saa saba.
Aidha Waziri mkuu Kassimu Majaliwa amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amewataka watanzania watanzania kuendelea kuwa wavumilivu na wastahimilivu katika kipindi hiki kigumu.
- Kisa cha Diana Chilolo kufuta namba ya Lowassa
- Tazama hapa msafara wa mwili wa Lowassa ukipelekwa Karimjee
- Shein, Sumaye waeleza uchapakazi wa Lowassa
- Picha: Matukio mbalimbali katika zoezi la kuaga mwili wa Lowassa
- Fredy Lowassa: Asingekuwa Rais Samia, baba asingefika juzi
- Read all related articles