Fri, 6 Sep 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Menejimenti ya mchezaji Yusuph Kagoma imeushukuru uongozi wa Yanga chini ya Rais Injinia Hersi Said kwa kumsamehe mteja wao ili aendelee kuitumikia Klabu ya Simba.
Yanga imeondoa shauri lake dhidi ya Kagoma katika Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF ambapo mchezaji huyo alishitakiwa kwa kufanya udanganyifu baada ya kusaini pamoja na kupokea sehemu ya malipo kutoka klabu ya Yanga lakini akaenda kujiunga na Simba.
Taarifa iliyotolewa na menejimenti ya Kagoma, imethibitisha kumalizika kwa sakata hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: