Waziri wa Habari,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amewataka watanzania kupuuza madai yanayoenezwa mitandaoni kuwa amepiga simu kwa baadhi ya vyombo vya Habari na kutoa maelekezo kwa vyombo hivyo kutochapisha waraka wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) unaohusu mkataba wa Uwekezaji Bandarini kwani hakuna ukweli wowote wa tuhuma hizo.
Waziri Nape amewaonya watu wanaotumia mitandao ya kijamii kuzusha habari za uongo kumhusu kwamba hawatafanikiwa.
"Ninawapa changamoto hawa wanaouzusha huu uongo,walete ushahidi wa mimi kupiga simu kwa vyombo vya habari na kuvieleza nini cha kuandika na niko tayari kuwajibika wakileta ushahidi huo"
- Ndani ya hukumu ya mkataba wa bandari ya Tanzania na DP World
- Tukisema tusiambiwe tunachanganya Dini na Siasa - Shoo
- Anna Tibaijuka amekosoa mkataba wa bandari hajakamatwa
- Hakuna mtu aliyekamatwa, atakayekamatwa kwa kukosoa mkataba wa bandari
- Wametishia kuipindua serikali – Nape
- Read all related articles