Yanga wemeweka historia ya kutinga kwa mara ya kwanza hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Yanga imetinga hatua hiyo baada ya kuifunga Rivers United kwa jumla ya mabao 2-0 ambayo waliyapa kwenye mchezo wa kwanza nchini Nigeria kabla ya kutoka suluhu kwa Mkapa.
Vijana hao wa Nasreddine Nabi watacheza dhidi ya Marumo Gallants F.C. ya Afrika Kusini kwenye hatua ya nusu fainali.
Timu zilizotinga nusu fainali kombe la Shirikisho Afrika
Yanga SC - Tanzania Asec Mimosas - Ivory Coast USM Alger - Algeria Marumo Gallants - Afrika Kusini
Droo ya nusu fainali CAFCC
Yanga SC vs Marumo Gallants
Asec Mimosas vs USM Alger
Yanga wataanzia nyumbani katika Uwanja wa Benjamin Mkapa mnamo Mei 10, 2023 kabla ya kurudiana na Marumo Gallants huko Afrika Kusini wiki moja baadae Mei 17, 2023.