Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

USM Alger watua Dar kibabe, waichimba mkwara mzito Yanga

Usm Alger Tree.jpeg USM Alger watua Dar, waichimba mkwara mzito Yanga

Fri, 26 May 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Kikosi cha klabu ya USM Alger ya Algeria kimewasili salama Jijini Dar es Salaam Tanzania ambapo kimepata mapokezi maalum na Balozi wa Algeria nchini Tanzania, Mheshimiwa Ahmed Jalal.

Balozi Jalal amewahakikishia kuwapatia vifaa na mazingira salama kuelekea mchezo wa mkondo wa kwanza wa fainali ya kombe la Shirikisho Afrika utakaopigwa Jumapili dhidi ya Young Africans SC ya Tanzania katika dimba la Benjamin Mkapa.

Akizungumza mara baada ya kuwasili, Kocha Mkuu wa USM Alger Denis Lavagne amesema hawana shaka na hali ya hewa na wamefika kucheza na Yanga na wamefanya maandalizi ya kutosha kwa ajili ya Fainali dhidi ya Yanga SC.

Kwa upande wake, Nahodha wa USM Alger amesema wamefanya mazoezi yao vizuri na wamejiandaa na kucheza kwenye mazingira ya joto na hawakuingia kwenye Fainali kwa bahati na wamefika Tanzania kupambana kwenye mchezo wa kwanza katika Uwanja wa Mkapa Jumapili.

USM Alger watakuwa na kibarua kigumu mbele ya Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania, Yanga kwenye mchezo wa kwanza wa fainali ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika utakaopigwa Jumapili katika dimba la Mkapa majira ya saa 10:00 jioni.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: