Tue, 24 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Michuano ya African Football League inaendelea hii leo, Simba inashuka dimbani kuikabili Al Ahly katika dimba la Cairo nchini Misri.
Mchezo wa awali ulimalizika kwa sare ya kufungana goli 2-2 uwanja waTaifa, leo Simba inahitaji ushindi au sare kuanzia magoli 3-3 ili ifuzu hatua inayofuata ya nusu fainali.
Ikitokea sare ya 2-2 italazimika kuchezwa mikwaju ya penalty, kama ikitokea sare ya 0-0 au 1-1 Simba itakuwa imeondoshwa rasmi kwa tofauti ya goli la ugenini.
Mnyama unguruma, umebeba bendera ya nchi
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: