Straika wa Mtibwa Sugar Matheo Anthony amesifu uwezo wa Mlinzi wa Simba SC Che Fondoh Malone licha ya wengi kumkosoa beki huyu katika mechi waliyokutana ya Ligi msimu huu.
Matheo alifunga mabao mawili lakini wengi wanasema magoli hayo yote yamefungwa baada ya makosa ya mlinzi huyo raia wa Cameroon.
Sasa Straika huyo wa Mtibwa amefungua kinywa chake na kumuelezea beki huyo,
“Che Malone ana uwezo mkubwa wa kuondoa mpira kwa haraka ndani ya 18 yao, ukiachana na hilo pasi anazotoa zinafika, anajua kumiliki mpira, mgumu na mkabaji kwelikweli ndiyo maana nasema akichanganya ataisaidia Simba SC“
Simba walishinda mchezo huo kwa magoli 4-1.