Tue, 23 May 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba imetoa mapumziko kwa wachezaji baada ya mechi za ligi kusogezwa mbele.
Simba ilipaswa kucheza na Polisi Tanzania siku ya Jumatano, Mei 24 lakini mchezo huo sasa utapigwa Juni 6 wakati mchezo wa kuhitimisha msimu dhidi ya Coastal Union utapigwa Juni 9.
Taarifa iliyotolewa na Simba imebainisha kuwa wachezaji watarejea mazoezini May 24 kwa ajili ya maandalizi ya mechi hizo ambazo ni za kukamilisha ratiba tu kwa Simba.
Simba imemaliza kwenye nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ikiwa imejihakikishia tiketi ya kushiriki michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika msimu ujao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: