Mon, 4 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Uongozi wa Simba SC leo Desemba 4 umetoa pole kwa familia zilizopoteza wapendwa wao katika maporomoko ya matope yaliyotokea jana wilayani Hanang mkoani Manyara.
Hadi kufikia leo asubuhi vifo 49 vimeripotiwa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga huku majeruhi wakiwa 85.
"Simba inaungana na Watanzania wote kuomboleza vifo vya wenzetu waliotangulia pamoja na kuwaombea majeruhi wapone haraka," imeeleza taarifa ya Simba
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: