Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Tanzania Prisons na kuchukua pointi tatu zikiwapandisha kileleni msimamo wa Ligi Kuu kwa pointi 12 kwenye mechi nne ilizocheza ikiwaacha Azam pointi 10 na Yanga 9.
Simba SC imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Tanzania Prisons na kuchukua pointi tatu zikiwapandisha kileleni msimamo wa Ligi Kuu kwa pointi 12 kwenye mechi nne ilizocheza ikiwaacha Azam pointi 10 na Yanga 9. Mabao ya Simba yamefungwa na Clatous Chama, John Bocco kipindi cha kwanza na la mwisho limefungwa na Saido Ntibazonkiza kwa mkwaju wa penalti huku la Prisons likifungwa na Edwin Barua.