Mon, 1 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba imetambulisha usajili wao Mpya wa kiungo, Saleh Karabaka kutoka Timu ya JKU ya Visiwani Zanzibar kwa mkataba wa miaka mitatu.
Karabaka mwenye umri wa miaka 23 anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Simba SC katika dirisha hili dogo la usajili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na waajiri wake hao wapya, Karabaka tayari amejiunga na kikosi hicho kwaajili ya michuano ya Mapinduzi Cup inayoendelea kutimua vumbi visiwani humo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: