Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Simba walifeli hapa kwa Raja Casablanca

Onyango 80333166541 Simba walifeli hapa kwa Raja Casablanca

Mon, 3 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mchezo wa juzi Jumamosi, dhidi ya Raja Casablanca, Simba kuna kitu walijaribu kukionyesha lakini changamoto kwao ni makosa yaliyofanyika kwenye safu ya ulinzi.

Pindi unapokutana na timu kubwa kama Raja Casablanca yenye wachezaji wakubwa kama wakina Amza Khaba lazima watatumia makosa yakoo kwa ufasaha watafunga mabao.

Simba SC wanaelekea hatua ya robo fainali hatua ambayo unakutana na timu nyinga zenye uwezo kama Raja ama zaidi ukifanya makosa kama yale utakuwa unajiweka kwenye wakati mgumu.

Mwalimu Robertinho anatakiwa kuja na mpango wa muda mfupi kuiandaa timu yake kwenye michezo mikubwa inayofwata ajaribu kuangalia namna ambavyo safu ya ulinzi inaweza kupunguza makosa.

Pia anatakiwa kuwa na mpango wa muda mrefu kwa maana ya kuanza kufwatilia mchezaji mwenye uwezo mkubwa na ataongeza nguvu kwenye safu ya ulinzi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: