Saidi Ntibanzokiza amefunga magoli matano (5) Simba SC ikiibamiza Polisi Tanzania 6-1 katika dimba la Azam Complex, Chamazi na kuishusha rasmi Daraja Timu hiyo kwa msimu wa 2022/23.
Kungo Mshambuliaji wa Simba Saidi Ntibanzokiza sasa amefunga magoli 15 kwenye NBCPL msimu huu (goli moja nyuma ya kinara Fiston Kalala Mayele.
Mabao mengine ya Simba yamefungwa na mlinzi Israel Mwenda huku lile la Polisi Tz likiwekwa wavuni na Henock Mayala.
Kwa ujumla Saido anaongoza kwa kuchangia magoli mengi zaidi Ligi Kuu (27) msimu huu (magoli 15 na asisti 12) kwenye Ligi kuu Bara.
Polisi Tz wanaungana na Ruvu kucheza Michuano ya Chmpionship msimu ujao.