Tue, 5 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha klabu ya Simba Kimeanza safari mchana huu kuelekea Morocco tayari kwa mchezo wao wa klabu Bingwa dhidi ya Wydad AC.
Mchezo unaovuta hisia za watu wengi ni kutokana na Vilabu vyote kuwa katika hali mbaya kimatokeo, Mchezo huo utachezwa disemba 9 - 2023 (Jumamosi), saa 4:00 Usiku kwa saa za Tanzania.
Simba wanahitaji Ushindi wao wa kwanza kwa msimu huu kimataifa na pia ili kufufua matumaini ya kwenda robo fainali huku Wydad wao wakihitaji kushinda ili kunusuru Ajira ya kocha wao mkuu na Mwenyekiti wa timu yao pia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: