Fri, 15 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Uongozi wa Klabu ya Al Ahly SC ya nchini Misri, umeomba Wachezaji wake wasijumuishwe kwenye timu ya taifa 'Misri' ili wajiandae na safari ya Tanzania dhidi ya Simba SC.
Al Ahly wanataka kutumia muda uliobaki kujiandaa na mchezo wa hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Simba SC utakaopigwa katika Uwanja wa Mkapa kati ya Machi 29-30.
Licha ya ombi hilo, uongozi wa Chama cha Soka nchini Misri haujatoa majibu mpaka hivi sasa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: