Mchambuzi wa masuala ya soka nchini kutoka East Africa Radio, Samwel Rashid mwenyewe anajiita Wakanda Republic amesema kuwa Klabu ya Simba bado inaishi kwenye kivuli cha kufungwa bao 5-1 na wapinzani wao Yanga.
Hii ni kutokana na uongozi wa timu hiyo kuendelea kutafuta mchawi aliyesababisha timu yao ikakandwa bao 5 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC mnamo Novemba 25, 2023.
"Naona Simba bado wanaishi kwenye kivuli cha bao 5 licha ya kwamba almost wiki tayari imeshaisha lakini bado wako kwenye ile tunasema hangover ya zile bao 5.
"Hii ni kwa sababu situation waliyonayo hivi sasa ni kama bado wanamtafuta mchawi aliyesababisha wao wafungwe zile bao 5, lakini kwenye scenario ya Football ni kitu cha kawaida kwa timu kufungwa bao 5," Wakanda Republic.