Wed, 15 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi cha Simba Queens kimefanikiwa kupata saini ya winga Diakiese Isabelle kutoka klabu ya Feminin Espoir kwa mkataba wa miaka miwili.
Diakiese anakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Simba Queens kuelekea kuanza msimu mpya wa mashindano 2023/24 ambao unatarajiwa kuanza Desemba 15.
Tayari winga hiyo amejiunga na wenzake kambini na anaendelea na mazoezi chini ya kocha Mussa Hassan Mgosi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: