Timu ya Simba Queens imefanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii kuelekea msimu mpya wa Ligi ya Wanawake Tanzania Bara baada ya kuifunga JKT Queens kwa penalti 5-4 kufuatia sare ya 1-1 leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
Timu ya Simba Queens imefanikiwa kutwaa Ngao ya Jamii kuelekea msimu mpya wa Ligi ya Wanawake Tanzania Bara baada ya kuifunga JKT Queens kwa penalti 5-4 kufuatia sare ya 1-1 leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam. JKT Queens walitangulia kwa bao la Stumai Abdallah dakika ya 15, kabla ya Danai Bhobho kuisawazishia Simba Queens dakika ya 24 mabao yote yakizalishwa na mipira ya kona.