Alhamisi ya Oktoba 5, 2023, Tanzania Prisons itaikaribisha Simba SC, kwenye mchezo wa raundi ya nne ya NBC Premier League ndani ya dimba la Sokoine jijini Mbeya.
Kuelekea mechi hiyo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amebainisha ya kwamba lengo lao la msingi kwa sasa ni kushinda mechi hiyo dhidi ya Tanzania Prisons na kisha mechi yao dhidi ya Singida Big Stars ambayo itapigwa Oktoba 8, 2023 mjini Singida.
“Akili na nguvu tumezielekeza kwenye michezo hiyo tukiwa na malengo ya kuendeleza ushindi kwenye ligi kuu ya NBC” ameandika Ahme Ally kupitia ukurasa wake wa Instagram.