Sat, 27 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Simba SC imefanikiwa kutwaa Kombe la Muungano baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Fainali usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzíbar.
Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, kiungo Msenegal, Babacar Sarr, dakika ya 77 akimalizia Moira wa adhabu uliopigwa na kiungo Mkongo, Fabrice Luamba Ngoma kufuatia mshambuliaji Mcameroon, Leandre Willy Essomba Onana kuangushwa nje kidogo ya boksi.
Hilo linakuwa taji la pili kwa Simba SC msimu huu baada ya kuanza na taji la Ngao ya Jamii wakimfunga mtani, Yanga Agosti mwaka jana Jijini Tanga.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: