Shabiki wa Simba Sc, Swaleh Madjapa amesema, kwa usajili ambao umefanywa na Mnyama katika dirisha hili kubwa la usajili, kama Simba haitachukua ubingwa msimu huu atapumzika kwa muda kufatilia ligi ya Bongo.
Madjapa anaamini wachezaji waliopo Simba na ambao wamesajiliwa kuelekea msimu mpya 2023|24, hakuna wa kuizuia Simba kuchukua makombe ya ndani.
Simba imesajili wachezaji wazuri wenye wasifu wa juu kwenye soka la Afrika, kila nikiangalia sioni sababu ya kushindwa kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu.
Una Ngoma, Onana, Kramo, Duchu, Kazi, Miquissone, Chama, Mzamiru, Kibu, Malone, Inonga, unakosaje kombe? Kwa wachezaji hawa tukikosa ubingwa, nitakaa pembeni kwa muda kushabikia soka la nchi hii.