Mchezaji wa zamani wa Klabu ya Simba Ismail Sawadogo ameweka wazi nia yake ya kuiburuza mahakamani Klabu ya Simba kufuatia kushindwa kumtimiza Makubaliano waliyowekeana wakati wanavunja Mkataba ambapo kwenye Mkataba ilikuwa wamlipe Mshahara wake wa miezi sita.
Mchezaji wa zamani wa Klabu ya Simba Ismail Sawadogo ameweka wazi nia yake ya kuiburuza mahakamani Klabu ya Simba kufuatia kushindwa kumtimiza Makubaliano waliyowekeana wakati wanavunja Mkataba ambapo kwenye Mkataba ilikuwa wamlipe Mshahara wake wa miezi sita. Sawadogo amesema viongozi wa Simba wamekuwa wanampiga Kalenda tu kwenye kumlipa fedha zake na mpaka sasa bado hawajamlipa hali iliyomfanya swala hilo alifikishe kwa Wanasheria wake ambao wamepanga kuishtaki Klabu ya Simba SC FIFA.