Klabu ya Simba imerudishwa tena nchini Morocco ambapo katika hatua ya robo fainali ya Kombe la Mabingwa Afrika imepangwa kucheza na mabingwa watetezi wa kombe hilo, Wydad Casablanca.
Simba ambaye ametoka kucheza kundi moja na Raja Casablanca ya huko huko Morocco, sasa ataanzia nyumbani katika Dimba la Mkapa na kumalizia nchini Morocco.
Simba SC vs Wydad Casablanca
Al Ahly vs Raja Casablanca
CR Belouizdad vs Mamelodi Sundowns
JS Kabyle vs ES Tunis
Droo ya nusu fainali:
Mshindi kati ya Kabyle na ES Tunis atakutana na mshindi kati ya Al Ahly na Raja Casablanca wakati mshindi kati ya Simba ma Wydad atakutana na mshindi kati ya Belouizdad na Mamelodi Sundowns.
Michezo ya robo fainali itapigwa tarehe 21 na 22 Aprili 2023 na marudiano ni tarehe 28 na 29 Aprili, 2023.