Mchambuzi wa masuala ya soka kutoka Wasafi FM, George Job amesema kuwa angekuwa kocha katika kikosi hicho basi angebaki na wachezaji wanne tu wa kigeni kati ya wachezaji 12 wanaosajiliwa kwa msimu.
Job amesema hayo akibainisha kuwa wachezaji wengi wa Simba wamechoka na hawana uwezo mkubwa uwanjani hivyo ni vigumu kuipa matokeo timu yao, badala yake wanatakiwa wasajiliwe wachezaji wengine wenye uwezo mkubwa zaidi.
“Kati ya wachezaji 12 wa kigeni pale Simba ningebakisha wachezaji wanne tu. Ningebaki na Inonga (Henock), Che Malone, Ngoma (Fabrice), na Baleke (Jean) kisha wengine wote ningewaacha,” amesema George Job.