Wawakilishi wa Tanzania katika Michuano mipya ya African Football League, Timu ya Simba imeanza safari jioni ya leo Oktoba 21 kuelekea nchini Misri kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa pili dhidi ya Klabu ya Al Ahly ya nchini Misri.
Simba inajiandaa na mchezo wa Robo Fainali ya mkondo wa pili wa michuano ya AFL, huku wakihitaji ushindi kutinga hatua inayofuata ama sare ya kuanzania magoli 3-3.
Mchezo wa Mkondo wa kwanza uliopigwa katika Dimba la Mkapa Oktoba 20 ulimalizika kwa sare ya magoli 2-2. Huku mchezo wa mkondo wa pili ukitarajia kupigwa Oktoba 24.
Kikosi kimeondoka na wachezaji 25 ambapo kitapita Ethiopia kabla ya kufika Misri. Mchezo utapigwa Jumanne saa 11 jioni jijini Cairo.
Tazama Picha hapa chini kuona msafara wa Kikosi cha Simba SC;