Thu, 19 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Fedha, Dk Mwigulu Nchemba kupitia akaunti yake ya Instagram amewaomba Watanzania kuwa wamoja katika mechi ya kesho Oktoba 20, Simba SC Tanzania dhidi ya Al Ahly SC ya michuano mipya ya African Football League.
Mechi hiyo itapigwa Uwanja wa Mkapa saa 12:00 jioni, Mwigulu amesema moja ya kipaumbele kama Mtanzania ni kuiombea Simba.
"Tuwaombee Simba, tuwaombee Simba, tuandike historia ya Taifa letu," -
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: