Wakati wengi wakihoji ni kwa namna gani Simba wamechangia ukarabati wa Uwanja wa Mkapa ambao unakwenda kufungua Michuano yenye hadhi kubwa Barani Afrika siku chache zijazo.
Hatimaye kitendawili kimeteguliwa na Naibu Waziri wa Michezo Hamis Mwinjuma "Mwana FA".
Akizungumza na East Afrika Redio Mwana F amesema;
"Katika ukarabati wa uwanja wa Mkapa Simba wamechangia kwa kuweka TV mpya pamoja na Fridge mpya"
"Hivyo kwa wanaoona kwamba Simba sports club hawatakiwi kuvimba (Wanafaidi) basi na wao watafute kitu cha kuleta ili wote wawe sawa kwani milango ipo wazi." - Hamisi Mwinjuma (MwanaFa),