Mon, 26 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki wa kushoto Yahaya Mbegu kupitia ukurasa wake wa instagram amechapicha ujumbe wa kuishukuru Ihefu “THANK YOU Mbogo Maji.”
Mbegu anahusishwa kujiunga na Simba kuchukua nafasi ya Gardiel Michael ambaye mkataba wake na Simba umemalizika na ameruhusiwa kuondoka.
Mbegu amekuwa kwenye kiwango kizuri tangu alipokuwa Polisi Tanzania, Geita Gold na Ihefu.
Singida Fountain Gate FC pia inatajwa kuwa kwenye mbio za kuwania saini ya mchezaji huyo aliyewahi kupita timu ya vijana ya Simba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: