Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mo Dewji: Simba mtaniua na Presha

Dewji1 Mohammed Dewji

Mon, 2 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Baada ya Simba kufanikiwa kufanikiwa kufuzu kwa hatua ya Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Power Dynamos ya Zambia katika Uwanja wa Chamazi.

Wengi wameonekana kuwa na mashaka na kiwango cha timu hiyo ambayo kwa miaka ya hivi karibuni imekuwa na ubora mkubwa katika Michuano ya CAF Afrika.

Simba imefanikiwa kufuzu kwa faida ya bao la ugenini baada ya kulazimiaha sare katika Dimba la Levy Mwanawasa ya magoli 2-2.

Hivyo sare ya mchezo wa jana inafanya matokeo kuwa 3-3 lakini Simba anakwenda Makundi kwa kuwa alipata magoli mengi ugenini.

Sasa mara baada ya mchezo kukamilika kwa sare ya bao 1-1 siku ya Jumapili Oktoba 1, Mwekezaji katika Klabu ya Simba SC Mohammed Dewji kupitia ukurasa wake wa X (twitter) ameandika;

"Dah, Jamani Simba Mtaniua na pressure".

Unadhani kipi kimemsukuma tajiri kuandika andiko hilo? Tupe maoni yako

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: