Mashabiki wa klabu ya Simba wamekuwa wakihamasika mara kwa mara endapo klabu imetengeza jambo kuelekea mchezo fulani, Leo klabu ya Simba imefanya Tamasha maeneo ya Coco Beach maalum kwajili ya mechi ye kombe la African Football League dhidi ya Al Ahly
Mashabiki wa Simba wana Imani kubwa na timu yao kuelekea mchezo dhidi ya Al Ahly, Mashabiki wamesha sahau yote ya nyuma ya timu kukosa muunganiko, timu kucheza bila kuvutia, Kupata matokeo kwenye hali ngumu yote mashabiki wameachananayo kutokana na mapenzi ya dhati na timu ya Simba
Kocha Robertinho na wachezaji wanatakiwa kujitoa kwa kiwango cha juu kwaajili ya kuthamini hali ya mashabiki na wadau wanaojitokeza katika hamasa na viwanjani kuiunga mkono klabu yao