Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mane apigwa faini ndefu Bayern

Sadio Mane Kupigwa Bei Bayern Mane apigwa faini ndefu Bayern

Wed, 19 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Baada ya Sadio Mane kumpiga mchezaji mwenzake wa bayern Munich, Leroy Sane wiki iliyopita nyota huyo amepigwa faini ya pauni 250,000, (Sh.724,445,000).

Pia inatajwa kuwa staa huyo raia wa Senegal yupo kwenye hesabu za kuuzwa mwishoni mwa msimu huu.

Mane alimchapa ngumi ya mdomo Sane kwenye chumba cha kubadilishia nguo wiki iliyopita kwa madai kuwa Sane alimkejeli kwa lugha na vitendo vya kibaguzi baada ya mchezo dhidi ya Manchester City.

Sane alionekana akiwa amevimba mdomo wakati Bayern Munich walipoivaa Hoffenheim wikiendi iliyopita na Mane hakuwepo kwenye mchezo huo wa Bundesliga.

Mane amesimamishwa kwa kitendo hicho huku akikatwa mshahara wake wa pauni milioni 17, (sh.49.2) kwa mwaka. Hii ni faini kubwa kwa Bayern Munich kutolewa katika historia yao.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: