Taarifa njema kwa mashabiki wa Simba na Tanzania ni kwamba mastaa wote muhimu wa Mnyama unaowajua leo hii watakuwa mazoezini kujiandaa na mechi dhidi Afircan Footbal League ya Al Ahly.
Traaifa kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa, ilibidi vigogo wa Simba wafanye harakati kubwa kuhakikisha kuwa mastaa sita wa kikosi kwanza cha timu hiyo ambao ni Clatous Chama, Henock Inonga, Kibu Denis, Mzamiru Yassin, Ally Salim, Israel Patrick Mwenda waliokuwa kwenye timu zao za taifa waanarejea kambini.
Michuano hiyo inayohusisha timu nane tu itaanza keshokutwa, Ijumaa, Oktoba 20, 2023 ambapo mchezo wa ufunguzi utakuwa kati ya Simba na AL Ahly majira ya saa 12:00 jioni katika Uwanja wa Mkapa.