Lameck Lawi ni kweli alikwisha saini kandarasi na Simba Sc na hata Picha za klabu za Utambulisho alikwisha piga,
Mvutano ulipo: Inasemekana sio viongozi wote waliohusika kwenye dili la kumuuza Mlinzi huyo wa kati kwenda Simba Sc,
Viongozi wengi wa Coastal Union wanatambua Lameck Lawi bado ni mchezaji wao kwakuwa walio wengi hawakuitwa kushirikishwa kwenye ishu hiyo ya kumuuza,
Nafahamu: Mpaka sasa na Simba Sc muda wowote wanaweza kumtambulisha Mlinzi huyo ili kuukata mzizi wa Fitna,
Malengo ya Viongozi wengi wa klab ya Coastal Union ilikuwa ni kumuuza Lawi kuanzia dirisha dogo la Usajili maana yake watakuwa wameshapata picha halisi ya Hatua yao waliyopo kimataifa,
Hofu ya Simba ndiyo iliyopelekea kumsaini mchezaji huyo Mapema zaidi ni vime alishakuwa kwenye rada za klab ya Azam na inafahamika mwezi januari huenda angejiunga nao.