Thu, 5 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kamati ya tuzo ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imemtangaza kocha wa KMC Abdihamid Moalin kuwa kocha bora wa mwezi baada ya kushinda michezo yote miwili KMC waliyocheza kwa mwezi Septemba.
Moalin amewashinda Roberto Oliveira wa Simba na Abdallah Mohamed wa Mashujaa baada ya kukusanya alama sita na kupanda kutoka nafasi ya 14 mpaka ya tano kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.
Aidha kamati imemtangaza meneja uwanja wa Azam Complex Amir Juma kuwa meneja bora wa uwanja kwa mwezi Septemba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: