Shomari Kapombe ana umri wa miaka 31, Zimbwe jr ana umri wa miaka 27, Ni mabeki waliocheza muda mrefu sana kwenye kikosi cha Simba na kupata nao mafanikio kwa muda mrefu bila kupata mbadala wao na kutopata mapunziko
Uongozi wa klabu ya Simba mara kwa mara wanatafuta mabeki wa kusaidiana na walinzi hao, Kibwana Shomari ni beki mwenye uwezo wa kucheza katika nafasi mbili tofauti anaweza kucheza upande wa kulia na pia upande wa kushoto
Umri wa Kibwana Shomari ni miaka 22 ni mchezaji ambaye anayeza kutumika kwa muda mrefu kwenye kikosi na kuisaidia Simba kwa muda mrefu, Kutokana na uzoefu na mafanikio aliyopata ndani ya Yanga kufika fainali ya shirikisho barani Afrika.