Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jean Baleke ajivisha mabomu Simba SC

Baleke Vs Jwaneng Glaxy.png Jean Baleke ajivisha mabomu Simba SC

Tue, 5 Dec 2023 Chanzo: Dar24

Mshambuliaji kutoka DR Congo Jean Baleke amewashusha presha Mashabiki na Wanachama wa Klabu ya Simba SC kwa kusema bado wana nafasi ya kusonga mbele kwenye Michuano ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika watakapoenda kusaka alama tatu dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco.

Mshambuliaji huyo aliyejiunga na Simba SC wakati wa Dirisha Dogo msimu uliopita 2022/23, amesema hadi sasa wana pointi mbili na wanaimani kubwa ya kupata pointi mchezo dhidi ya wenyeji wao, Wydad Casablanca ugenini ili waweze kufikisha pointi tatu muhimu kwa ajili ya kufikia malengo yao.

Baleke amewaomnba msamaha Mashabiki na Wanachama wa Simba SC kwa matokeo ya nyuma na kuwataka kuungana kuwa nguvu mmoja kuelekea kwenye mechi hiyo dhidi ya Wydad Casablanca.

Amesema wachezaji wanatambua umuhimu wa mchezo huo, na kwamba wanahitaji kufanya vizuri kwa sababu malengo yao ni kuona Simba SC inasonga mbele kuvuka makundi na kucheza Robo Fainali.

“Samahani mashabiki wetu, tusahau matokeo yaliyopita ambayo kocha wetu (Abdelhak Benchikha) amefanyia kazi mapungufu yetu sasa nguvu na akili zetu tumezielekeza kusaka ushindi dhidi ya Wydad Casablanca,” amesema Baleke.

Kuhusu tetesi za kutakiwa kurejea katika klabu yake ya TP Mazembe, Baleke amesema bado yupo na ni mtoto wa Simba, anachokifikiria zaidi ni kuona timu yake inafanikiwa kuvuka katika hatua ya makundi na kwenda robo hatimaye nusu fainali.

Simba SC wanatarajia kushuka dimbani Desemba 9, mwaka huu, wakiwa ugenini dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco, mchezo utakaochezwa katika Uwanja wa Grand stade de Marrakech, uliopo Marrakech, saa 4:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Chanzo: Dar24
Related Articles: