Mlinzi wa kati wa klabu Simba Hussein Kazi inatajwa kuwa ni sehemu ya kukamilisha dili la Usajili la Mlinzi wa kati wa klabU ya Coastal Union Lameck Lawi,
Simba imetoa Kiasi cha pesa pamoja na Hussein kazi ili kukamilisha dili hilo ambalo lilikuwa la wengi kuelekea soko la usajili.
Haikuwa rahisi kwa klabu ya Coastal Union kutupilia mbali ofa za Vilabu vya Ihefu na Azam FC ambao nao walituma ofa ya kumtaka Lameck Lawi.
Hussein Kazi amesajiliwa na Simba mwanzoni mwa msimu huu, ambapo alitazamiwa kutoa ushindani kwa wachezaji wa kikosi cha kwanza kwenye timu hiyo hali ambayo ni kama imeshindikana huku Simba wakijipanga kurudisha makali yao.