Wakati Kiungo kutoka Nigeria akitoa shutuma nzito kwa uongozi wa Simba SC ambao wametangaza kuachana nae.
Okwa amezungumza mambo mengi ambayo amekutana nayo akiwa Simba kubwa ni lile la kukosa nafasi ya kucheza akidai kuwa kocha sio anaepanga Timu klabuni hapo.
Sasa Mchambuzi wa michezo kutoka Clouds Fm, Edgar Kibwana amefunguka ya moyoni kumzungumzia mchezaji huyo.
Edgar anasema;
"Okwa sio mchezaji wa kiwango mpaka kufikia hatua ya kutuhamishia mada, kama angekuwa mkali namba angepata tu haijalishi timu anapanga nani, alipaswa kuondoka kimya kimya kama mwenzake Dejan tungemuelewa maana hana kiwango cha kusema ageuke gumzo"