Mshambuliaji wa kimataifa wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, Chris Mugalu ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa Simba Sc amesaini mkataba wa mwaka 1 kujiunga na Klabu ya Al Washm SC ya Saudi Arabia kama mchezaji huru baada ya mkataba wake na Klabu ya Al-Quwa Al-Jawiya ya Iraq kumalizika.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, Chris Mugalu ambaye alikuwa mchezaji wa zamani wa Simba Sc amesaini mkataba wa mwaka 1 kujiunga na Klabu ya Al Washm SC ya Saudi Arabia kama mchezaji huru baada ya mkataba wake na Klabu ya Al-Quwa Al-Jawiya ya Iraq kumalizika. Mugalu tayari ameanza kuwatumikia waajiri wake wapya na jana alifanikiwa kufunga goli 1 kwa timu yake ya Al Washm katika mchezo wa ligi daraja la pili.