Nyota wa Simba SC, Clatous Chota Chama ameomba kuungana katika nyakati hizi ambazo kumekuwa na minong’ono ya hapa na pale tangu kumalizika kwa #DerbyYaKariakoo Novemba 5. 2023.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Chama ameandika “Katika nyakati hizi hakuna haja ya kunyoosheana vidole na kutupiana lawama, haitotusaidia kwa namna yoyote ile. Huu ni wakati sahihi wa kushikamana pamoja na kuunganisha nyoyo zetu. Twendeni tena leo tukiwa na nguvu moja na kufanya kazi ili kurejea katika ari yetu”
Mnyama leo atashuka dimbani kuvaana na Namungo FC katika muendelezo wa mikikimikiki ya NBC Premier League.