Mpaka sasa umri wa Juma Nyoso ni miaka 39, Lakini inashangaza kuona anavyopambana uwanjani na wachezaji wachanga na wenye umri wenye sifa za kuwa na nguvu na kasi uwanjani, Jambo ambalo mabeki wa Simba wanakosa hasa kwa Che malone
Ukiangalia kuanzia msimu wa juzi akiwa Geita gold alikuwa katika kiwango bora hasa dhidi mechi kubwa Azam, Simba na Yanga ikapelekea mpaka wana mbogp maji Ihefu kushawawishika kumsajili
Msimu uliopita alikuwa katika kiwango bora sana tena wengi tunakumbuka jinsi alivyoweza kumzuia Fiston Mayele katika mchezo dhidi ya Yanga na kuibuka na ushindi, Hata katika mchezo dhidi ya Yanga alifanya kazi nzuri na pacha wake leny Kisu kuwazui washumbuliaji wa Yanga
Unapokwenda kucheza mechi za kimataifa na mabeki kama Che malone, Inonga, hussein kazi ambao mara nyingi hawawezi kupambana na washambuliaji wenye sifa za kuwa na kasi na nguvu na akili kubwa ya kufunga ni ngumu kufanikiwa na hapo ndipo unapohitaji mtu wa aina ya Nyoso.