Jina la nahodha wa Simba, John Bocco ni kati ya majina mawili yaliyopendekezwa kumrithi aliyekuwa Meneja wa timu hiyo, Patrick Rweyemamu ambaye amepewe majukumu mengine kwenye upande wa timu za vijana.
Jina la Bocco na mratibu wa timu hiyo Abbas Suleiman ndio wanatajwa huku mabosi wa Simba wanataka Bocco ndiye awe Meneja kutokana na ushawishi alionao na ukaribu kwa wachezaji baada ya kuwaongoza kwa muda mrefu kama nahodha wao.
Hata hivyo mbali na mvutano wa pande mbili juu ya jina la Bocco, inadaiwa nyota huyo bado anataka kucheza soka akiamini ana uwezo mkubwa wa kuendelea kufumania nyavu.