Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bingwa Ligi ya Wanawake kupatikana Iringa leo

SIMBA QUEENS LEOOZ Bingwa Ligi ya Wanawake kupatikana Iringa leo

Wed, 17 May 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ligi Kuu ya Wanawake inahitimishwa leo ambapo timu zinazoangaliwa ni Simba Queens na JKT Queens zenye nafasi ya kuchukua ubingwa wa ligi hiyo.

Simba yenye mataji matatu ya Ligi Kuu ina pointi 42 katika nafasi ya pili ikitarajiwa kucheza na Ceasiaa Queens kwenye Uwanja wa Chuo Kikuu cha Mkwawa huku JKT ikiumana na Mkwawa Queens, Uwanja wa Samora, viwanja vyote viwili vikiwa mkoani Iringa.

Iwapo Simba itashinda itakuwa kwenye nafasi ya kutangazwa mabingwa lakini ikitegemea na matokeo ya JKT inayoshika nafasi ya kwanza kwenye msimamo kwa pointi 43 ambao wakitwaa leo itakuwa ni ubingwa wao wa tatu kibindoni.

JKT itapepetana na Mkwawa wanaoshika mkia kwa pointi tatu wakati mpinzani wa Simba, Ceasiaa wanashika nafasi ya sita kwenye msimamo wakiwa wameshajihakikishia kubaki wakiwa na pointi 21.

Mkwawa ni kama imeshashuka daraja haina cha kupoteza hivyo uwezekano wa JKT kushinda ni mkubwa ingawa mpira unaweza kubadilika kulingana na maandalizi.

Michezo mingine ya leo ni Alliance Girls dhidi ya Baobab Queens kwenye Uwanja wa Nyamagana, Mwanza, Fountain Gate Princess dhidi ya the Tigers Queens kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma na Aman Queens itapepetana na Yanga Princess kwenye Uwanja wa Ilulu, Lindi.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: