Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Benchikha: Sitaki historia ijirudie chini yangu

Benchikha Mapinduzi.jpeg kocha Abdelhak Benchikha

Tue, 27 Feb 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wakati Simba wakijipanga kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mchezo wa mwisho hatua ya Makundi Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Jwaneng Galaxy.

Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha amesema kuwa hataki historia mbaya ya Simba dhidi ya Jwaneng Galaxy.

Akizungumza kuelekea mchezo huo Benchikha anasema;

“Galaxy sio timu rahisi ni kama jeshi lisilotabirika, hakuna aliyedhani kama ingeifunga Wydad Casablanca nchini Morocco kwenye mchezo wa kwanza wa makundi, hata hapa Simba rekodi zinaonyesha wamewahi kushtua kwa kushinda hapa, nadhani mashabiki na hata wao wachezaji wanalijua hili na tayari nimeshakaa kikao na wachezaji na kuwakumbusha,”

“Kwenye soka mambo ya kushtua kama haya huwa yanatokea, sitaki historia hii ijirudie hapa chini yangu, nimezungumza nao tukiwa kule ugenini juzi nadhani kila mtu ataelewa tulizungumza nini. Tunatakiwa kujipanga na vita nzito ya mchezo huu, nawaomba mashabiki wetu waje kwa wingi kuwapa hamasa wachezaji wao wakiwa vitani ndio kitu pekee tunahitaji kutoka kwao,”

“Ili kushinda tunahitaji kufunga mabao ya kutosha lakini pia kujilinda vizuri lakini kule mbele bado hatujawa imara zaidi tutawaongezea wachezaji mbinu za kutengeneza nafasi na kuzitumia kwenye hizi siku tutakazokuwa kambini.” Kuonyesha msisitizo, kocha huyo hajawapumzisha wachezaji.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: